
Katika upande wa ukwasi sokoni hapo upande wa hisa umeongezeka kwa shilingi bilioni 4 ikiwa ni ongezeko la asilimia 3.7 kwa mujibu wa ripoti iliyowasilishwa na meneja uendelezaji biashara Leonald Kameta ambaye amebainisha mchango na ushiriki mkubwa kwa kampuni za ndani umezidi kuimarika
“Kwa hali ilivyo sasa kwenye ukubwa wa mtaji sokoni hapo umeongezeka hasa kwa wiki iliyoishia desemba 2,2022 kutokana na kuongezeka kwa bei za makampuni kadhaa za ndani”amesema Leonald
Kuhusu uwekezaji kwenye hati fungani zile za miaka 20 zimeonekana kupendwa zaidi kutokana malengo ya wawekezaji.