Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwanjali azua hofu Msimbazi

Jumatatu , 13th Feb , 2017

Beki kisiki wa kati tegemeo wa Simba, Mzimbabwe Method Mwanjali yuko hatarini kuukosa mchezo dhidi ya mahasimu wa jadi, Yanga Februari 25, mwaka huu.

Beki kisiki wa kati wa Simba Method Mwanjali akitibiwa.

Miamba hiyo ya soka nchini, Simba na Yanga itavaana katika mechi ya Mzunguko wa Pili wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara Jumamosi ya Februari 25 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwanjali anaweza kuukosa mchezo huo baada ya kuumia katika mechi nyingine ya Ligi Kuu dhidi ya Prisons ya Mbeya, Simba wakishinda 3-0 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mwanjali aliye katika msimu wake wa kwanza Simba SC, alitolewa kwa machela na nafasi yake kuchukuliwa na kiungo Mwinyi Kazimoto katika dakika ya 62.

Meneja wa Simba SC, Mussa Hassan Mgosi amesema kwamba kuna muda mrefu kabla ya mechi na Yanga na hatarajii maumivu ya Mwanjali yatakuwa makali kiasi cha kumuweka nje Februari 25.

“Naona muda bado upo sana, tena wa kutosha. Sitarajii kama atakuwa ameumia kwa kiasi kikubwa,” alisema Mgosi.

Taarifa zaid kutoka klabuni humo zinadai kuwa daktari wa timu amesema huenda Mwanjali akaanza mazoezi mepesi wiki ijayo, lakini haina uhakika kwa asilimia kubwa kama ataweza kuwa fiti hadi Februari 25.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto