Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Miyeyusho ayeyushwa kwa KO huko Jamhuri ya Czech

Jumatatu , 4th Jul , 2016

Ile desturi ya mabondia wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania kutofanya vema nje ya nchi katika mapigano yao ya kirafiki na kimashindano imeendelea tena mara baada ya bondia Francis Miyeyusho naye kupoteza pambano la ubingwa wa UBO ugenini nchini Czech

Bondia Francis Miyeyusho 'chichi mawe'.

Bondia wa ngumi za kulipwa nchini Tanzania Mtanzania Francis Miyeyusho maarufu kama 'Chichi Mawe' mwishoni mwa juma lililopita alishindwa kuipeperusha vema bendera ya taifa baada ya kupoteza mpambano wake wa kimataifa wa raundi 12 kuwania ubingwa wa mabara wa UBO International akipambana na bondia toka nchini Czech.

Miyeyusho ambaye ni mkazi wa Kinondoni jijini Dar es Salaam alipoteza mpambano huo baada ya kupigwa kwa technical knock out (KO) na mpinzani wake Martin Parlagi katika mpambano uliopigwa mjini Plague Jamhuri ya Czech.

Kwa mujibu wa mratibu wa ndani wa mpambano huo katibu mkuu wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST) Antony Rutha amesema bondia huyo 'Chichi Mawe' alipoteza mpambano huo mapema katika raundi ya pili tu mara baada ya kupigwa ngumi ya tumbo na kujikuta akishindwa kuendelea na mpambano huo baada ya kuhisi maumivu makali ya tumbo na hivyo kumlazimisha mwamuzi kusimamisha mpambano huo na kumpa ushindi bondia Martin Parlag na kutwaa mkanda huo wa UBO kwa Mabara.

Kipigo hicho kinakuwa ni moja ya mwendelezo wa mabandia wengi wa ngumi za kulipwa nchini kushindwa kutamba katika mapambano wakiwa ugenini na kimsingi wadau wa ngumi wakiwemo mabondia wenyewe na viongozi wao na makocha wanatakiwa kujiuliza wapi wanajikwaa ama wanaangukia na kujikuta wakishindwa kufua dafu katika mchezo huo wakiwa ugenini.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala