Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mchenga BBall Stars yawakalisha TMT

Jumamosi , 19th Aug , 2017

Mchenga BBall Stars wamefanikiwa kuwachapa wapinzani wao TMT kwa pointi 87-82 mchezo wa tatu kati ya mitano katika fainali ya Sprite BBall Kings uliyopigwa katika viwanja vya Don Bosco Oysterbay Jijini Dar es Salaam.

Nahodha wa Mchenga BBall Stars Mohamed Yusuph akimuwekea kizingiti mchezaji kutoka TMT, Erick Lugora.

Kutokana na matokeo hayo timu ya Mchenga BBall Stars imeweza kurudisha furaha kwa mashabiki zao baada ya kupoteza mechi iliyopita katika fainali hizi za Sprite BBall Kings kwa kuchapwa kwa pointi 87-78 na mpinzani wake TMT.

Pamoja na hayo, mechi ya leo iliweza kuonyesha utofauti mkubwa katika mechi zote zilizowahi kuchezwa katika michuano hii, kutokana na wachezaji wa pande zote mbili kuonyesha umahili wao waliyokuwa nao katika kucheza pamoja na kushambulia.

Mamia ya mashabiki waliyoweza kujitokeza kutazama mtanange wa fainali za Sprite BBall Kings leo Don Bosco Oysterbay 

Kwa upande mwingine, mchezaji Erick Lugora kutoka TMT ameweza kuibuka 'best scorer' kwa pointi 23 akifuatiwa na Marcelo Nyirabu kutoka Mchenga BBall Stars kwa kupata pointi 18 katika mechi ya tatu ya fainali za Sprite BBall Kings.

Mchenga na TMT zitakutana tena Agosti 23 (Jumatano) ya mwaka huu kucheza game 4 ambapo mchezo huo kwa upande mmoja utaweza kuwa wa mwisho endapo Mchenga BBall Stars akiweza kufunga tena.

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto