Siku kadhaa baada ya kuanza kwa kambi ya mazoezi kwa ajili ya matayarisho ya msimu mpya, tayari imethibitishwa kuwa kikosi cha Mbeya City FC kitasafiri hadi mkoani Morogoro kwa ajili ya mchezo wa kujipima nguvu dhidi ya wenyeji Mtibwa Sugar kwenye uwanja wa Jamhuri Julai 30, mwaka huu.
Hii ni mara ya pili kwa Mtibwa na City kucheza mchezo wa kirafiki awali ikiwa ni msimu uliopia ambapo timu hiyo kutoka Manungu iliibuka na ushindai wa bao 1-0 lililofungwa kipindi cha pili na Mohamed Ibrahim.
City inatarajia kuondoka Mbeya Julai 28 tayari kwa mchezo huo uliopangwa kupigwa siku ya jumamosi ya mwisho wa mwezi huo.





