Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mashabiki wa Liverpool washambuliwa Ukraine

Ijumaa , 25th Mei , 2018

Hofu ya usalama katika mji wa Kiev nchini Ukraine, imeongezeka baada ya mashabiki wawili wa timu ya Liverpool kushambuliwa na genge la wahuni ikiwa imebaki siku moja kabla ya mchezo wa fainali wa mashindano ya klabu bingwa Ulaya.

Gazeti la Independent limeandika kuwa, Polisi nchini Ukraine, wamethibitisha tukio hilo na kudai kuwa wa mashabiki wawili wa Liverpool wamejuruhiwa katika ya mji wa Kiev mahali ambapo kundi la mashabiki hao walikuwa wamewasili katika mgahawa wa Rooster Grill.

Polisi wameongeza kuwa watu wawili wanashikiliwa kufuatia tukio hilo ingawa wengi wao walifanikiwa kukimbia katika eneo la tukio. Mmoja wa mshabiki Liverpool, Jason Frost amethibitisha kushambuliwa masaa mchache baada ya kuwasili katika mji huo 

“Tulikuwepo hapa kwa masaa manne  na kisha baadae tukaanza kushambuliwa, walikuja  kama kundi la mbwa, ilikuwa inaogopesha sana, tulikuwa tunapata chakula cha jioni, sikuja hapa kwa mambo haya, bali nilikuja kuangalia mpira” amesema Bwana Frost.

Kesho Mei 26, timu ya Liverpool kutoka England itakabiliana na Real Madrid ya Hispania katika mchezo wa mashindano ya klabu bingwa Ulaya utakaofanyika mjini Kiev katika nchi ya Ukraine.

HABARI ZAIDI

Maduka ya Wafanyabiashara yakiwa yamefungwa

Wamiliki wa maduka Mebya wafunga biashara zao

Kamanda wa Polisi mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Agustino Senga

Polisi waambiwa kazi yao ni kazi ya Mungu

Kiwanda cha sukari Mtibwa

11 wafariki dunia kiwanda cha Mtibwa

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC Kapenjama ataka uaminifu kwa wakulima Songea

Bashiri Mohamed (35) Mwenye Koti Jeusi akiwa anafikishwa Mahakamani Ilemela, Jijini Mwanza

Aliyezini na binti yake apandishwa kizimbani

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania

Wanahabari wasisitizwa kuzingatia maadili ya kazi

Wilman Kapenjama Ndile, Mkuu wa Wilaya ya Songea

DC atangaza msako kuwaondoa walinzi wazee kazini