Manula ameonekana kwenye picha ya pamoja akiwa anafanya mazoezi pamoja na magolikipa wengine wa Simba SC Ahmed Feruzi, Abel Hussein, Ally Salim na Ayoub Lakred ikiwa ni kwa mara ya kwanza akionekana akifanya mazoezi ya pamoja, siku za nyuma alikuwa akifanya mazoezi binafsi yap eke yake.
Simba imerejea mazoezini jana Alhamisi Oktoba 12,2023 ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kikosi hicho kuelekea kwenye mchezo wa African Football League dhidi ya AL Ahly mchezo utakaochezwa Oktoba 20, 2023.