Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Manchester City yaendeleza balaa usiku wa mabingwa

Alhamisi , 25th Feb , 2021

Matajiri wa jiji la Manchester nchini England, klabu ya Manchester City imeendeleza mwendo wake wa ushindi na sasa kufikisha ushindi wa michezo 19 mfululizo kwenye michuano yote baada ya usiku wa jana kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Borrusia Moenchengladbach.

Wachezaji wa Manchester City wakimpongeza Bernardo Silva baada ya kufunga bao la kwanza usiku wa jana.

Ushindi huo unawafanya Manchester City kuwa na faida ya mabao mawili ya ugenini na kuwa na uwezekano mkubwa wa kutinga hatua inayofuata ya Robo fainali ya michuano ya klabu bingwa Barani Ulaya kuelekea mchezo wake wa mkondo wa pili unaotaraji kuchezwa tarehe 16 Machi mwaka huu.

Mabao ya City yamefungwa na kiungo Bernardo Silva na mshambuliaji wake Gabriel Jesusu na kuweka rekodi ya kufunga kwenye michezo yake yote mitano ya hatua ya 16 bora ya michuano hiyo katika misimu yake minne akiwa na Manchester City.

Kwa upande mwingine, licha ya timu hiyo ya Wananchi wa jiji la Manchester 'The Citizens', kuutawala mchezo kwenye maeneo yote lakini kocha wa timu hiyo, Mhispania Pep Guardiola hakuonekana kuridhishwa na idadi hiyo ya mabao.

“Kiujumla, tuliutawala mchezo. Haikuwa bahati hatukuwa sahihi vyakutosha kuweza kuzitumia nafasi za mabao tulizozitengeneza. Hiki ni kitu ambacho tunapaswa kukiboresha kwenye michuano hii. Kwenye michuano hii inapswa uwe na usahihi wa hali ya juu ili uhakikishe unasonga mbele”.

Katika kujibia nafasi ya City kuwa bingwa wa michuano hiyo baada ya kuwa na mwendo mzuri, Pep amesema “Nilipoiona Bayern Munich jana sikuwezi kufikiria hivyo. Kwasasa naifikiria Westham United . Kama watu wanasema hivyo inabidi tukubali, sio tatizo, tunakubali”.

Mabingwa watetezi, Bayern Munich ilipata ushindi wa mabao 4-1 ugenini dhidi ya Lazio ya Italia usiku jana.

Manchester City jumamosi ya kesho kutwa tarehe 27 Februari 2021, inatazamiwa kushuka dimbani kukipiga na 'Wagonga nyundo wa jiji la London' klabu ya Westham United kwenye ligi kuu nchini England.

Manchester City wakipata ushindi basi wataifikia rekodi ya kushinda michezo 20 mfululizo kwenye michuano yote kama walivyofanya mwaka 2017.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto