Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

KMC kutolewa chambo na Simba, Yanga, Azam FC

Ijumaa , 23rd Aug , 2019

Kuanzia leo Ijumaa hadi Jumapili ya wiki hii, mashabiki wa soka Tanzania wana kazi moja tuu ya kuhakikisha timu nne zinafuzu katika hatua ya pili ya michuano ya vilabu barani Afrika.

Wachezaji, makocha na viongozi wa KMC

Leo KMC itashuka dimbani kucheza mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho dhidi ya AS Kigali katika uwanja wa taifa, ambapo katika mchezo wa kwanza mjini Kigali, timu hizo zilitoka sare ya kutofungana bao lolote.

Katika msimu wake wa kwanza katika Ligi Kuu Tanzania Bara, KMC imefanikiwa kucheza michuano mikubwa barani Afrika huku ikifanikiwa kupata udhamini mkubwa wa Shilingi Bilioni moja, ambao ni historia kwa klabu hiyo.

Pia kesho Jumamosi, Azam FC itawakaribisha Fasil Kenema katika uwanja wake wa Chamazi Complex baada ya mchezo wa awali nchini Ethiopia kumalizika kwa Azam Fc kupoteza kwa bao 1-0. Yanga itakuwa ugenini nchini Botswana dhidi ya Township Rollers ambapo katika mchezo wa awali, timu hizo zilitoka sare ya kufungana bao 1-1.

Simba itawakaribisha UD Songo, Jumapili ya Agosti 25 katika uwanja wa taifa baada ya mchezo wa awali nchini Msumbiji kumalizika kwa sare ya kutofungana.

Akizungumza kuelekea mchezo huo,  Mwenyekiti wa Bodi ya KMC, Benjamin Sitta amesema, "kuna kazi kubwa ya kufanya kwa KMC ila jambo la kwanza ni matokeo kisha mengine yatafuata, wachezaji wanajua wameahidiwa kitu gani, ni jambo la kusubiri".

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto