Jumatatu , 11th Jul , 2016

Bingwa wa dunia mchezo wa magari ya langa langa, Lewis Hamilton ametwaa taji la British Grand Prix, baada ya kumaliza kinara, mwishoni mwa wiki iliyopita, huko Silverstone.

Bingwa wa dunia mchezo wa magari ya langa langa, Lewis Hamilton ametwaa taji la 4 la British Grand Prix, baada ya kumaliza kinara hapo jana huko, Silverstone.

Ushindi huo unamfanya Hamilton, abakishe pointi 1 kumfikia dereva mwenza Mercedes, Nico Rosberg katika kinyanganyiro cha kuwania ubingwa wa dunia.

" Sijui kama unaweza kuwa na furaha kama niliyo nayo mimi".Alisema Hamilton, baada ya mbio hizo.