Jumanne , 4th Mei , 2021

Naibu Waziri wa Utumishi na Utawala Bora Deo Ndejembi, amesema kuwa serikali inatambua uwepo wa rushwa katika sekta ya michezo hususani katika suala la ukataji wa tiketi ambapo ameitaka TFF kuanza kukata tiketi kwa njia ya mtandao badala ya ule wa awali uliozoeleka.

Naibu Wazxiri, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Deo Ndejembi

Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 4, 2021, jijini Dodoma wakati akijibu maswali ya mbunge wa Mlalo, Abdallah Shangazi, kuhusu uwepo wa rushwa katika sekta ya michezo, huku akiongeza kuwa licha ya kuchukua hatua mbalimbali ya kuziba mianya rushwa bado pia wataendelea kuwachukulia hatua watuhumiwa wote wa rushwa katika sekta hiyo.

"Ili kuziba mianya ya rushwa niwaase TFF na timu za mpira wa miguu waachane na tiketi zile za kuchana na waweze kwenda kwenye 'electronic ticket' hii itasaidia sana upungufu na upotevu wa mapatao, itaongeza mapato kwa timu zao lakini vilevile kwa TFF", amesema Ndejembi

Aidha ameongeza kuwa "Imeonekana kuwa ikiwa timu ya Simba inacheza uwanja unajaa sana, lakini bado mapato yanakuwa ni hafifu ukilinganisha na timu nyingine ambayo ni kubwa Afrika Mashariki na kati"