Alhamisi , 3rd Sep , 2015

Mabingwa wa Kombe la Kagame, Timu ya Azam FC imesema mchezo wao wa kirafiki dhidi ya Ruvu Shooting utakaochezwa hapo kesho uwanja wa Mabatini mkoani Pwani utakuwa wa mwisho kwa ajili ya kuelekea kwenye msimu mpya wa ligi kuu ya soka Tanzania Bara.

Afisa habari wa Azam FC Jaffary Maganga amesema, hawawezi kucheza mechi nyingine tena maana michuano ya ligi kuu inaanza wiki ijayo hivyo kuwa na mechi wana uwezo wa kupata majeruhi suala ambalo litamchanganya kocha.

Maganga amesema, wataondoka na wachezaji wote walionao kambini ili kocha kuweza kuangalia viwango vya wachezaji vilipofikia tangu kuanza kwa mechi za maandalizi ya ligi hiyo.