Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Mwasiti atoa wito kwa Nandy na Zuchu

Jumanne , 5th Jul , 2022

Staa wa bongo fleva, Mwasiti Almasi leo alifika katika ofisi za East Africa TV na East Africa Radio na kukabidhi mchango wa taulo za kike pakiti 72 kupitia kampeni ya Namthamini ambazo zitakwenda kusaidia wanafunzi 7 shuleni kwa mwaka mzima.

Mwasiti akiongea kwenye kipindi cha Mama Mia cha East Africa Radio siku ya leo.

Mwasiti ni miongoni mwa wasanii waliokuwepo katika uzinduzi wa kampeni ya Namthamini iliyofanyika Mei 27 mwaka huu katika shule ya sekondari Kidete, Wilaya ya Kigamboni, Dar es Salaam.

Hedhi imekua kikwazo kikubwa sana katika elimu ya mtoto wa kike, kwani wapo wanaoshindwa kwenda shule siku 3 hadi 7 kwa sababu ya maumivu makali wakati wa hedhi, na wengine kwa sababu ya ukosefu wa taulo za kike za kujihifadhi hivyo anaweza kubaki nyumbani hadi amalize hedhi.

Mwasiti anasema anatambua changamoto wanazokumbana nazo wanafunzi wa kike shuleni wakikosa taulo za kike za kujihifadhi katika kipindi cha hedhi, moja wapo ni kushindwa kufika shule.

Kampeni ya Namthamini imelenga kuwasaidia wanafunzi wanaotoka katika familia duni nchini kwa kuwapatia taulo za kike na kuhakikisha hawakosi tena masomo pindi wanapokuwa katika siku zao za hedhi na kuwaongezea uwezo wa kujiamini, kusoma kwa bidii na kutimiza ndoto zao.

Mwasiti ametoa wito kwa wasanii wa kike nchini kama Linah, Nandy, Dayna Nyange, Maua Sama, Haitham, Saraphina na Zuchu wajitokeze kuwasaidia wanafunzi wa kike waweze kupata mahitaji muhimu shuleni.

 

 

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala