
Mratibu wa onyesho Solomon Nasuma akizungumza na waandishi wa habari
Akizungumza hii leo jijini Dar es Salaam, Mratibu wa onesho hilo Solomon Nasuma, amesema wamewachagua wasinii hao kutokana na kuwa na sifa ya kuweza kufanya show ya live, ambapo siku ya onesho hilo kutakuwa na Live Band kwa wasanii hao.
Katika kuonesha anajipanga vyema na show ya Live Band, msanii wa kimataifa wa Tanzania Nasib Abdul maarufu kama Diamond, alikuwa akijifua vyema kwa ajili ya mazoezi ya kufanya muziki wake Live na bendi.
