Jumatatu , 24th Aug , 2015

Nyota wa muziki Vanessa Mdee, ameeleza namna ambavyo anamhusudu mama yake akiwa ni mfano bora ambao anafahamu kabisa kuwa akiuiga ataelekea kuwa mtu bora kabisa katika maisha yake.

Nyota wa muziki nchini Vanessa Mdee,

Hii ni kauli aliyoitoa sambamba na maelezo tata kuwa kuna mambo mengi sana ambayo ametofautiana naye kitabia.

Bila kueleza kwa undani zaidi ni mambo gani hayo ambayo anatofautiana na mama yake, Vanessa ameeleza kwa upande mwingine kuwa Mama yake ni Mcha Mungu, na mpenda watu akiwa na uwezo mkubwa kabisa wa kupika na kuelewana na watu.