Ijumaa , 5th Aug , 2016

Msanii wa Bongo Fleva Udeude aliyefariki dunia tarehe 4 mwezi Agost mwaka huu amezikwa katika makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia tarehe 5.

UDE UDE (Enzi za uhai wake)

Marehemu ameacha mke na mtoto huku baadhi ya watu wake wa karibu pamoja na Bob Junior, Bonge la Nyau na muandaaji wa muziki wa Bongo Fleva Alonem ambaye ndiye aliyekuwa wa mwisho kufanya kazi wakiongoza mazishi.

Mungu awatie nguvu ndugu, jamaa pamoja na wadau wote wa tasnia nzima ya muziki wa bongo fleva nchini. Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi Amin.