Alhamisi , 7th Aug , 2014

Wabunifu mahiri wa mavazi hapa Tanzania, Twins Fashion ambao huwatengenezea wasanii mavazi ya kuvaa jukwaani, wamekiri kuanza kuona mafanikio ya kazi hii ambayo sasa imeanza kuvuka mipaka na kuitangaza mitindo ya Tanzania.

wabunifu wa mitindo ya mavazi nchini Tanzania Twins Fashion

Twins Fashion ambao kwa mafanikio makubwa wamekwishawahi kufanya kazi ya kumvalisha msanii Diamond Platnumz na Makomandoo kati ya wengine, wamesema kuwa mitindo yao ambayo hubuni wenyewe, ina lengo la kuleta changamoto pia kwa wabunifu wengine ndani na nje ya Tanzania.

Wabunifu hawa pia wameiambia e-newz kuwa hivi sasa wameingia mkataba na msanii Jose Chameleone katika kazi ya kumtengenezea aina mbalimbali ya mitindo ya mavazi.