
Nyota Ndogo ametoa ujumbe huo kwa kuandika kwenye ukurasa wake wa Instagram, na kusema kwamba iwapo mtu atamuona binti yake amebananishwa na mwanaume, asimuache aendelee kufanya hayo na badala yake amchape ili kumpa fundisho, kwani watoto ni wa wote.
“Mukimuona Barka amekua mkubwa, umkute amebanwa ukutani na mwanamume ama kijana na amevaa nguo za shule chukua fimbo tandika huku ukimuuliza kwenu wapi, mlete nyumbani kwangu ukimwambia maisha magumu sana kwanini unataka kuyaharibu”, ameandika Nyota Ndogo.
Nyota Ndogo ameendelea kwa kusema kwamba ni vyema kuzungumza na watoto na kuwaonya, pia wazazi washirikiane katika malezi kwani hata kama sio wako wa kumzaa.
