Alhamisi , 7th Dec , 2017

Baada ya kuenea  kwa picha katika mitandao ya kijamii  za Muingizaji na Msanii Zuwena Mohamed,maarufu kama Shilole zikionyesha kuwa amefunga ndoa na mpenzi wake Uchebejana usiku , aliyekuwa mpenzi wa Shilole, Nuh Mziwanda ametuma dongo.

Nuh Mziwanda ameandika ujumbe katika ukurasa wake wa Instagram ambao unatafsiriwa kama amebeza ndoa hiyo.

Mpenzi huyo wa Zawadi wa Shilole, Nuh Mziwanda ameandika,

"Aliyelala na bibi harusi wiki moja kabLa ya harusi’, na wala sio bwana harusi bado mnanishauri harusi, (all girls are pretenders )."

Siku chache zilizopita  Shilole alisisitiza kuwa atafunga ndoa kabla ya mwaka huu kuisha japo watu walimbeza, hayawi hayawi yamekuwa.