Ijumaa , 5th Jun , 2015

Rapa Nas ameungana na jarida la kimataifa la The Guardian kutoka Marekani kutangaza namna nchi nyingine kutoka sehemu mbalimbali duniani ikiwepo Uganda iliyopo Afrika Mashariki, zina upendo na utamaduni wa Hip Hop na Break Dancing.

Nas

Hii ni kupitia makala ya video yenye dakika 6, ikihusisha mijadala ya vijana juu ya jinsi ambavyo Hip Hop inamaanisha katika jamii zao ambazo zinakabiliwa na umasikini, na kuonesha kuwa nyuma ya picha mbaya inayotolewa na vyombo vya habari, jamii hizi zina vijana walio na utajiri wa utamaduni huo.

Nchi nyingine ambazo zinahusika katika makala hiyo ni pamoja na Colombia, Yemen pamoja na Cambodia.