Ijumaa , 27th Jun , 2014

Meneja ambaye pia ni mwimbaji wa bendi maarufu ya muziki wa dansi jijini Dar es
Salaam 'The Kalunde Band', mwanadada Deborah Nyangi, ameongea na eNewz kuhusu kipaji cha binti yake ambaye anaamini siku moja atafuata nyayo zake katika muziki.

Mwimbaji wa bendi ya Kalunde nchini Tanzania, Deborah Nyangi

Deborah amegundua kuwa mwanae anayeitwa Florence Florenso siku zote ambazo anakuwa akimlea anaonyesha kuwa ana kipaji cha kupiga kinanda kitu ambacho kinamvutia mtoto huyo.

Aidha Deborah anayefanya vyema kwa kutoa video yake inayotamba hivi sasa katika stesheni mbalimbali nchini iliyobatizwa jina "Fingo', ameongezea kuwa anatarajia kutoa ngoma yake mpya inayopikwa na prodyuza C 9, huku akijianda kutoa albamu yake mpya itakayowashirikisha wanamuziki mbalimbali nchini.

Mwanamuziki, Tanzania, Deborah Nyangi, Kalunde Band