Ijumaa , 27th Jan , 2017

Msanii wa taarabu Khadija Kopa amewasihi mameneja kujitokeza kuwadhamini na kuwasimamia wasanii wa taarabu ili waweze kufanikisha muziki wa tarabu kufika kimataifa.

Khadija Kopa

Akipiga story kupitia eNewz ya EATV Khadija Kopa amesema kwa sasa anahitaji kupata wadhamini ili kuweza kufanya video nzuri kwani yeye anajua kuimba lakini hajui maswala ya uongozi hivyo anatamani kupata usimamizi ili kuweza kutengeneza kazi nzuri zaidi.

Pia amemalizia kwa kusema  kwa sasa anajipanga ili arudi na muziki wa kisasa na kuwasihi mameneja wanaotamani kufanya kazi na yeye wajitokeze wasiogope umaarufu wake.