
Kaligraph
Rapa huyu ambaye muziki wake umeanza kueleweka kwa kasi sasa, amesema kuwa kutokana na hali kuwa ngumu alikuwa anafanya kazi ya uchekeshaji ambayo ilikuwa ngumu sana kukubalika na watu katika kipindi cha mwanzoni.
Kaligraph amesema kuwa, anajivunia kutoka alipotoka na ameweka wazi kuwa kukulia kwake huko Kayole Kenya kumekuwa na mchango mkubwa katika muziki wake na ujumbe anaojaribu kufikisha kwa wapenzi wa muziki wake.