Jumanne , 11th Mei , 2021

‘Ukifika lazima upimwe’ hii ni kauli aliyoitoa Harmonize akiwa uwanja wa ndege wa Mwl. Julius Nyerere leo akitokea Nigeria na wasanii wenzake wa Konde Gang.

Pichani wasanii Harmonize kushoto na Janjaro kulia

Kauli hiyo inatafsiriwa kama dongo kwa Rapper Dogo Janja baada ya wiki iliyopita kugoma kufanyiwa vipimo vya COVID-19 akiwa uwanja wa ndege Dar es Salaam alipowasili toka Afrika Kusini.

 
Kupitia vipande vya video ambavyo ameviweka kwenye insta story yake, Harmonize pamoja na wenzie wamesikika wakisema kwamba majibu yao yapo negative wakiwa na maana kuwa hawana Corona.