
Msaani Dogo Janja
Hayo yote yamekuja baada ya msanii Dogo Janja kuweka ujumbe ndani ya mtandao huo akisema “Sina Urafiki na Dunia Yenu!” Kauli iliyopata komenti za wadau wengi wakisema.
Sina urafiki na Dunia YENU!
— Dogo Janja (@dogojanjatz) September 21, 2018
Irene anakutosha dunia tuachie na sie tusio na marafiki
— Eddo (@edward_mkumbata) September 21, 2018
www.eatv.tv imemtafuta Dogo Janja kuelezea hayo ambapo amesema, kauli hiyo inatoka katika wimbo wake mpya anaotarajia kuachia hivi karibuni,unaoenda kwa jina la “ “IMANI” huku akikataa kuzungumzia mahusiano yake na Irene Uwoya na kusema kauli hiyo haihusiani na maisha ya ndoa yake kwa sasa.
Kushindwa dumu wewe kunywa sumu Mimi sitaku hukumu nitatoa tu rambirambi
— Fundikira jr (@Hamadon14) September 21, 2018
Tumekuwa tukishuhudia kuwepo kwa matukio yanayopelekea watu wengi kujiua hususani watu maarufu duniani kutokana na “stress” hofu za maisha au mahusiano. Wasanii Avicii na Mac miller ,waliripotiwa kupoteza maisha kutokana na stress walizokuwa nazo ndani ya mahusiano yao.
Dogo Janja amedaiwa kutokuwa na mahusiano mazuri na mpenzi wake Irene Uwoya, hali inayoashiria kuvunjika kwa ndoa ya wawili hao.