Jumatatu , 19th Jan , 2015

Shavu kubwa kabisa la kufanya onesho katika ufunguzi wa mashindano ya AFCON ambalo amelipata msanii Eddy Kenzo kutoka Uganda mwishoni mwa wiki, limefanikiwa kumuongezea msanii huyu heshima na pia mashabiki wengi kutoka nje ya mipaka ya nchi yake.

msanii Eddy Kanzo wa nchini Uganda

Staa huyu anayetamba kupitia ngoma yake ya 'Sitya Loss', ameweza kushiriki jukwaa moja na wasanii wakubwa Afrika, akiwepo Kenzo, Manni Bella, Tofan, Singuila na WizKid kati ya wengine, ikiwa ni moja ya maonesho yake makubwa kabisa kuwahi kufanya.

Star huyu anaweka rekodi ya kuwa msanii pekee kutoka Afrika Mashariki aliyeshiriki katika wimbo wa Hola Hola, ambao ni wimbo rasmi wa mashindano ya AFCON, nafasi ambayo ameitumia vizuri kupiga hatua nyingine katika upande wa muziki wake kimataifa.