Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Yanga maarufu 'rais wa Tanga' ahukumiwa miaka 30

Ijumaa , 20th Nov , 2020

Mahakama ya Uhujumu Uchumi, imemuhukumu kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka 30 mfanyabiashara Yanga Omari, maarufu kama rais wa Tanga,baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kusafirisha na kuuza madawa ya kulevya aina ya Heroin kiasi cha gramu 1052.63.

Mahakama Kuu Kanda ya Tanga

Akitoa hukumu hiyo Jaji Imaculata Banzi wa Mahakama hiyo, amesema ameridhika na ushahidi uliotolewa, ambapo upande wa mshtakiwa uliowakilishwa na Mohamed Kajenge uliiomba mahakama impunguzie adhabu  kwa sababu ni kosa lake la kwanza na  ana umri mkubwa zaidi ya miaka 60 na anategemewa na familia yake huku pia akidaiwa kuwa na shinikizo la damu.

Hata hivyo, Jaji Banzi amesema gari aina ya Land-Cruser V8 na silaha yake vilivyokuwa vikishikiliwa na serikali virejeshwe kwa familia yake ikiwemo madawa aliyokamatwa nayo yateketezwe mara moja.
Yanga anadaiwa kwamba mnamo Agosti, 2018 na wenzake  wawili walikamatwa mtaa wa Bombo jijini Tanga, wakitaka kusafirisha dawa hizo za kulevya.

Faraja Nchimbi ambaye ni Mkurugenzi Msaidizi  kutoka, ofisi ya Taifa ya mashtaka ambaye pia anasimamia mashauri mbalimbali na masuala yanayohusiana na dawa za kulevya, ugaidi pamoja na masula ya makosa ya baharini, amesema kuwa uamuzi huo ni sehemu ya jitihada ya serikali katika kuhakikisha vita dhidi ya dawa za kulevya inapiganiwa vilivyo kwa kuzingatia sheria kali zilizopo.
 

HABARI ZAIDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa January Makamba

Ziara ya Rais Samia Korea kuanza rasmi Mei 31 2024

Bw. Nazar Nicholas (katikati) akikabiziwa tuzo ya WSIS 2024

Tanzania yashinda Tuzo WSIS 2024, nchini Uswisi

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20