Ijumaa , 24th Jun , 2016

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron amesema ataachia madaraka mwezi Oktoba, mwaka huu kufuatia Mataifa ya Umoja wa Kifalme wa UK, kupiga kura ya kujitoa Umoja wa Ulaya (EU).

Waziri Mkuu wa Uingereza David Cameron akiongea nje ya Downing Street

Katika taarifa yake aliyoitoa nje ya Ofisi za Downing Street, Cameron amesema atajaribu kuliongoza jahazi la taifa la Uingereza kwa wiki chache zijazo na miezi, lakini kiongozi mpya anahitaji sasa.

Waziri Mkuu Cameron alikuwa akiwasihi wananchi kutojitoa Umoja wa Ulaya, alishindwa kwa kura asilimia 52 dhidi asilimia 48 licha ya London, Scotland na Ireland ya Kaskazini kunga mkono kubakia EU.