
Dk. Self Rashid ametoa wito huo kupitia katika hotuba yake iliyosomwa na mkuu wa wilaya ya Chunya Deodatus Kinawiro kwenye maadhimisho ya siku ya chama cha msalaba mwekundu duniani ambayo kitaifa yamefanyika jijini Mbeya
Kwa upande wake makamu wa Rais wa chama cha msalaba mwekundu nchini Tanzania Dk. Zainab Gama amesema chama cha msalaba mwekundu kimekuwa kikifanya kazi zake bila upendeleo kwa kutoa misaada ya
kibinadamu wakati wa majanga, huku akiitaka serikali kupitia wizara ya sheria na katiba kutunga muswada wa marekebisho ya sheria ili upitishwe na bunge na hatimaye kuwa sheria itakayosaidia chama chicho kufanya kazi zake kwa ufanisi zaidi.