
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega
Waziri Ulega ametoa maelekezo hayo wakati akizindua Bodi ya Nne ya Ushauri ya Wakala ya Mafunzo (LITA) na Bodi ya Wakurugenzi ya Ranchi za Taifa (NARCO) jijini Dar es Salaam
"Huu ndio uwe mtazamano wetu, kijana anapofundishwa na kumaliza mafunzo yake pale LITA nyie NARCO muweke utaratibu wa kutenga maeneo kwa ajili ya kuwapa vijana hao ili wajifunze kwa vitendo ufugaji wa kisasa, hatutaki kufundisha watu ili waende kuhangaika bali waingie katika biashara ya mifugo na mazao yake," amesema Waziri Ulega
Aidha, aliwataka LITA kuhakikisha wanakuwa na mkakati wa kuwaunganisha vijana hao na taasisi za kifedha kwa ajili ya kuwajengea uwezo wa kuwapa mbinu za kutekeleza mkakati wa kibiashara na kupata mitaji.
Halikadhalika, ameielekeza NARCO kuhakikisha wanaweka mikakati ya kuvutia wawekezaji na kuhakikisha wanakuwa kinara wa biashara ya nyama nchini.