Picha za tukio la ajali
Taarifa iliyotolewa na Mganga Mkuu wa wilaya ya Ngara Dr. Revokatus Dyekobora amesema kuwa tukio hilo limetokea leo majira ya asubuhi wakati wafanyakazi hao wakielekea kazini kwao eneo la Rusumo na kusababisha ajari.
Amesema kuwa hadi sasa majeruhi 20 wamelazwa katika hospitali ya Murgwanza na kati ya hao wawili hali zao ni mbaya na wanatarajiwa kupelekwa hospitali ya Bugando kwa matibabu zaidi, huku katika hospitali ya Nyamiaga kukiwa na majeruhi wengine 15.
Pamoja na hayo Dk. Dyekobora ameomba watu wajitokeze kutoa damu kwa ajili ya majeruhi hao kwa kuwa damu nyingi inatuika ili kuoko maisha ya majeruhi, hivyo wasamaria wema wanaombwa kufika katika hosipitali ya Miruganzwa pamoja na ile ya Nyamiaga.
Kwa upande wake Mkuu wa jeshi la Polisi mkoani Kagera, Bw. Revocatius Malimi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba jeshi linaendelea kufanya uchunguzi wa ajali hiyo na kwamba taarifa zaidi zitatolewa na kamanda wa polisi Mkoani Kagera .




