
Kamanda wa polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja Kamishna msaidizi wa jeshi hilo ACP Daniel Shillah amesema watuhumiwa hao watano wamehusika na wizi wa nyaya hizo na wengine kushiriki kuiba magaloni ya mafuta ya dizeli, ambayo yameibiwa kwenye sehemu mbili tofauti ikiwemo kwenye ujenzi wa hotel na barabara.
Aidha Kamanda Shillah amebainisha kuwa wataendelea kuilinda miradi ya serikali kutokana na serikali kuwekeza kiasi kikubwa cha fedha katika kukamilisha miradi hiyo.