Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Wananchi Bukoba waondokana na adha ya maji

Jumanne , 21st Mar , 2023

Baadhi ya wakazi wa vijiji vitatu kati ya vitano vilivyoko katika kata Karabagaine katika wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, wameondokana na adha ya kutembea umbali mrefu kwenda kuchota maji kwenye vyanzo vya asili, na kuepuka ugomvi uliotokana na kugombania maji,

Hii ni baada ya mradi wa maji kuanza kutoa huduma katika vijiji hivyo

Wakizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji katika kata hiyo ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya maji, wakazi hao ambao ni kutoka katika vijiji vya Kitwe, Itahwa na Kiziru wamesema kuwa walipata matumaini baada ya serikali kuanza utekelezaji wa mradi huo

"Maji haya yametukomboa, tulipata shida sana hasa akina mama na pia  watoto ambao walitoka shule badala ya kupata muda wa kujisomea walipoteza muda mwingi kufuata maji mtoni, lakini pia tulikuwa tunafikia hatua ya kugombana yaani tunapigana kwa sababu ya maji hasa wakati wa msimu wa kiangazi" wamesema wananchi

Mhandisi Gadama Kulwa ni msimamizi wa mradi wa maji Karabagaine ambao unatekelezwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Bukoba - BUWASA - akitoa taarifa ya mradi huo amesema kuwa hadi kukamilika kwake utagharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.8

"Mradi huu utahudumia vijiji vitano wa Kata ya Karabagaine ambavyo ni Kitwe, Itahwa, Kiziru, Kangabusharo na Ibaraizibu, vyenye wakazi 16,104" amesema mhandisi Kulwa

"Hadi kufikia mwezi Machi mwaka huu, jumla ya vijiji 560 kati ya vijiji 660 vinavyosimamiwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini -RUWASA- vinapata huduma ya majisafi na salama, ambapo zaidi ya wakazi milioni 2.1 wananufaika" amesema mhandisi Gerome

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto