Alhamisi , 18th Jul , 2024

Wanafunzi wawili wa darasa la saba wa shule msingi Mahaha iliyopo halmashauri ya mji wa Bariadi wamekufa maji wakati wakiogelea kwenye dimbwi lililokuwa limejaa maji.

Wanafunzi hao ni Anna Mayunga (14),Martha Dickson (13) wote wakazi wa Bariadi na tukio hilo limethibitishwa na mkuu wa wilaya ya Bariadi Simon Simalenga huku akitaka uchunguzi wa kina ufanyike juu ya tukio hilo.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Simon Simalenga amesema watoto waliopoteza maisha walikuwa wanatarajia kufanya mtiani wa darasa la saba

Katika hatua nyingine mkuu wa wilaya ya Bariadi Simon Simalenga akasema suala la ulinzi wa mtoto ni la jamii nzima.