Jumapili , 27th Nov , 2016

Wanafunzi wa kike 141 katika baadhi ya shule za msingi na sekondari katika wilaya ya Muleba mkoani Kagera wamesitisha masomo yao baada ya kupata ujauzito wa katika kipindi cha kuanzia 2012 hadi mwanzoni mwa mwezi Machi mwaka huu.

Hayo yameelezwa na mkuu wa wilaya ya Muleba Bw Richard Ruyango wakati wa uzinduzi rasmi wa kitabu cha wanafunzi ambao ulifanywa na mkuu wa mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salmu Mustafa Kijuu zenye lengo la kutokomeza mimba za utotoni na maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi.

Mkuu huyo wa wilaya ameelezea matatizo yanayochangia matatizo yanayochangia mimba za utotoni ni pamoja na uwajibikaji mdogo wa wazazi wa watoto wenye wanafunzi kuwafichia siri wanaowapa ujauzito.

Kufuatia tatizo hilo mkuu wa mkoa wa Kagera Meja Jenerali Salmu Mustafa Kijuu  ameagiza viongozi kuanzia ngazi ya vijiji katika mkoa huo kuunda kamati ambazo zitakua zinashirikiana na club za wanafunzi zinazoundwa katika kutokomeza vitendo hivyo.

________________
Kumpigia KURA msanii unayempenda kwenye #EATVAwards Bofya hapa https://www.eatv.tv/awards