
Waokoaji wamekuwa wakitumia mikono yao mitupu kuchimba kwa ajili ya manusura.Vifaa vya uokoaji haviwezi kupita barabara zilizozuiwa na boulders kufikia vijiji vya mbali karibu na kitovu katika Milima ya Atlas.
Wengi wanalala katika magofu huku wenyeji wakisubiri kwa hamu misaada.Serikali ya Morocco imesema imekubali msaada kutoka nchi nne hadi sasa - Uingereza, Uhispania, Qatar na Umoja wa Falme za Kiarabu.
Tetemeko la ardhi la Ijumaa, ambalo ni baya zaidi katika kipindi cha miaka 60, lilipiga chini ya vijiji katika milima ya Atlas kusini mwa Marrakesh.
Katika kijiji kimoja cha Tafeghaghte, taarifa zinasema wakazi 90 kati ya 200 walithibitishwa kufariki na wengine wengi hawajulikani walipo.
Kwa mujibu wa takwimu ya awali ilikua 2,122 lakini serikali imesema kuwa huenda ikafikia 2,500.
Watu wengine 2,476 wamejeruhiwa, ambapo idadi ambayo imeongezeka kutoka 2,400 ya waliojeruhiwa.