Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Waislamu washerehekee Eid hivi- Sheikh Alhad

Ijumaa , 14th Mei , 2021

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum amesema mtu yeyote anayekusudia kufanya maasi katika siku ya Eid anadhihirisha ni kwa jinsi gani alikuwa hajafunga bali kushinda njaa kwa siku 30.

Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum

Akizungumza katika mahojiano na kipindi cha East Africa Radio Sheikh Alhad amesema uaminifu uliokuwepo katika kipindi chote cha mfungo wa  Ramadhani unatakiwa uendelezwe katika shughuli zote na maisha kwa ujumla.

"Muislamu anatakiwa kuyaendeleza aliyojifunza katika mwezi wa ramadhani, mtu ambaye amejipanga kufanya maasi siku ya Eid, huyu ni mtu ambaye anaonyesha dalili kwamba funga yake ilikuwa ni patupu, alikaa tu na njaa muda wote wa siku 30" amesema Sheikh Alhad 

"Sisi waislamu hatutakiwi tujipange kwa ajili ya kutenda maasi kwa ulevi, au kwa matendo machafu mbalimbali, ni jambo lisilofaa na linaonesha watu hawajaelewa lengo na dhumuni la mfungo wa ramadhani" aliongeza Sheikh Alhad

Akizungumzia namna ya kusherehekea sikukuu hii ya Eid al-fitr, Sheikh Alhad amewataka waislamu kusherehekea kwa kuchunga mipaka ya Mwenyezi Mungu na kuwasisitizia wazazi kuwapeleka watoto katika maeneo salama na yasiyo hatarishi.                                                                                                        

"Namna ya kusherehekea ni kwa kuchunga mipaka ya Mwenyezi Mungu, watu waende maeneo yanayofaa, tuwapelekee watoto wetu maeneo salama na si hatarishi, mabinti wetu wasichaganyike na wavulana katika fukwe na kurudi saa nne usiku," amesema Sheikh Alhad

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto