
Waziri wa Elimu Profesa Adolf Mkenda
Akifungua ushirikiano huo Waziri wa Elimu Prof Adolf Mkenda amesema Tanzania na China zinaushirikiano wa muda mrefu kwenye sekta mbalimbali ikiwemo uchumi,siasa na sasa uwekezaji huu umeelekezwa kwenye sekta ya elimu katika vyuo vya ufundi ili kuwasaidia watanzania vijana kupata wataalam ambao watafanya kazi miradi mbalimbali.
"Tuko na vyuo vingi vya ufundi sasa ni kweli wenzetu wachina wameendelea sana katika teknolojia hivyo kupitia utaratibu wa vijana kwenda huko kusoma watakuwa na vigezo vya kuajirika kirahisi zaidi na tayari vijana kadhaa wameanza kwenda kutoka vyuo vya ufundi kadhaa," amesema Prof Mkenda
Hata hivyo kwa upande wao Baraza la Taifa la Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET)amesema hii leo tayari vyuo 30 mbalimbali vya ufundi kutoka China vimehudhuria katika semina ya kujadili na kuingia mikataba ya awali na vyuo mbali mbalimbali vya ufundi kutoka hapa Tanzania.
"Kwa wanafunzi ambao wanasoma degree watapata fursa ya kusoma miaka miwili china na mingine miwili Tanzania ambapo ndani ya shahada yake ndani yake atakuwa ngazi ya diploma ya ufundi kutoka China ambayo ataweza kuajirika hapa kwenye makampuni yao," amesema Adolf Rutayugwa-Katibu Mtendaji NACTVET.