Mkuu wa mkoa wa Simiyu, David Kafulila
Amesema Tanzania ina kiwango cha chini cha umaskini dhidi ya wananchi wake, ikilinganishwa na mataifa mengineyo ya ukanda wa nchi za Afrika Mashariki, ambapo ameeleza kuwa kufanya kazi kwa bidii, maarifa na nidhamu ya kazi ndiyo kielelezo cha mafanikio ya kiuchumi ulimwenguni kote.
RC Kafulila ameyasema hayo wakati wa kongamano lililoandaliwa na vijana wa Mkoa wa Simiyu, wanaosoma vyuo vikuu nchini, lililolenga kujadili masuala ya ajira, elimu na uchumi.