Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Urithi wa Mkapa kwa Watanzania

Alhamisi , 31st Dec , 2020

Usiku wa kuamkia Julai 24, 2020, Tanzania ilipata pigo kubwa baada ya kuondokewa na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin William Mkapa, aliyefariki dunia katika moja ya hospitali zilizopo ndani ya jiji la Dar es Salaam, taarifa ambazo zilitolewa na Rais Dkt. John Magufuli.

Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Hayati Benjamin William Mkapa, wakati wa uhai wake.

Tanzania ilizizima, mataifa mbalimbali Duniani yaliomboleza na Taifa hili, haikuwa jambo rahisi kwa Rais Dkt. John Magufuli, kutangaza taarifa za kifo cha mtangulizi wake huyo katika madaraka, lakini ombi lake kwa Watanzania lilikuwa ni moja tu kuwa waendelee kuwa watulivu na wamoja katika kipindi hicho cha majonzi makubwa.

Huo ulikuwa ni msiba mwingine mkubwa wa kitaifa baada ya ule wa aliyekuwa Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambao ulitokea Oktoba 14, 1999, na katika kipindi chote cha maombolezo bendera zote zilipepea nusu mlingoti.

Rais Mkapa, alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 81, na kuzikwa kijijini kwao Lupaso, Masasi mkoani Mtwara, ikumbukwe tu alifariki ikiwa imepita miezi takribani nane, tangu alipozindua kitabu chake alichokipa jina la "My Life My Purpose", ambacho kilizinduliwa katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) na Rais Dkt. Magufuli na kuhudhuriwa na marais wengine wastaafu Dkt. Jakaya Kikwete, Mzee Ali Hassan Mwinyi na viongozi wengine.

Mkapa ambaye alizaliwa mwaka 1938 mjini Ndanda, alihitimu shahada yake ya kwanza katika Chuo Kikuu Cha Makerere nchini Uganda na baadaye Chuo Kikuu cha Columbia, ambapo alipata shahada ya uzamili katika taalumu ya mahusiano ya umma, alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuanzia mwaka 1995  hadi 2005.

Wakati wa uhai wake amewahi kupata nyadhifa mbalimbali katika ngazi ya mikoa na serikali ya Tanzania zikiwemo Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, Wizara ya Mambo ya Nje na katika utawala wake kama Rais, pamoja na masuala mengine ya jitihada za upatanishi atakumbukwa na hatua za ubinafsishaji wa mashirika ya umma nchini.

HABARI ZAIDI

Baadhi ya Majirani wa Kijana Amani Abed ambaye Amejinyonga baada ya kutoka Hospitali.

Kijana ajinyonga baada ya kutoka hospitali

Antony Blinken, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani

Marekani yatangaza kulifadhili jeshi la Ukraine

Kaimu Mkurugenzi wa ufuatiliaji na uzingatiaji sheria NEMC,

Wamiliki wa Hospitali nchini wapewa siku 90

Baadhi ya Wakazi wa Kata ya Madanga Mkoani Tanga

Wagoma kubeba mimba kwa kukosa huduma za afya

Mkuu wa mkoa wa Songwe Daniel Chongolo

Wanafunzi 194 washika mimba ndani ya mwezi mmoja

Mabaki ya gari aina ya Noah iliyopata ajali Morogoro

Ajali yachukua uhai wa watu saba Morogoro

Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba

Wawekezaji wawekeze sekta za uzalishaji - Nchemba

Muonekano wa Kiburugwa ambako Nyumba zaidi ya Tisa Zimebomolewa na Maporomoko ya Tope

Maporomoko ya udongo yasomba nyumba 9 Mbagala