Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Upinzani kupoteza majimbo muhimu, inamaana gani?

Ijumaa , 30th Oct , 2020

Katika mwendelezo wa matokeo ya uchaguzi uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, kumeshuhudiwa sura mpya kutoka Chama cha Mapinduzi (CCM),katika majimbo yaliyoonekana na kuaminika kuwa ni ngome za vyama vya upinzani ikiwemo chama kikuu cha upinzani CHADEMA

Kushoto ni Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, wa pili ni Kiongozi Mkuu wa ACT Wazalendo, Zitto Kabwe.

Miongoni mwa majimbo hayo ni pamoja na jimbo la Hai, Moshi Mjini, Mbeya Mjini, Arusha Mjini, Iringa Mjini, Ubungo, Tarime Mjini, Tarime Vijijini na Kawe.

Pengine mwanzoni ilikuwa vigumu kufikiria kuwa majimbo hayo yangetoka katika mikono ya vyama vya upinzani kwa wakati mmoja na katika uchaguzi mmoja lakini kwa sasa kama yupo aliyefikiria hivyo ni dhahiri kuwa wakati umepingana na fikra zake.

Kushoto ni Esther Matiko, kati ni Esther Bulaya na kulia ni Halima Mdee

Je ngome hizo za upinzani kuwa chini ya CCM inamaanisha nini ? '' Maeneo hayo kupoteza ni kwa sababu Chama Cha Mapinduzi kimewekeza nguvu kubwa kwa maaana kwanza nguvu yenyewe ya Magufuli kama Rais wa Jamhuri ya Muungano, Amiri Jeshi Mkuu na msimamizi mkuu wa watumishi lakini jambo la pili unaweza kujiuliza suala dogo tu inawezekanaje CCM imeweza kushinda jimbo kama Hai alafu imeweza kushindwa Jimbo kama Mtwara Mjini kwa Hawa Ghasia kwa hiyo ni maswali ambayo yanakuwa na tafakuri nyingi sana'' amesema Mbwana Allyamtu, Mchambuzi wa Siasa za Kitaifa na Kimataifa.

Aidha Mbwana ameongeza kuwa '' Hatuwezi kusema kuwa ni ushindi wa CCM ila ni ushindi wa Dk. Magufuli kwa sababu katika kampeni zake amekuwa akihimiza mara nyingi kwamba anahitaji wabunge wa Chama Cha Mapinduzi ili aweze kuleta maendeleo''

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto