Jumamosi , 8th Mei , 2021

Mahakama ya wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, imemhukumu Semeni Gwewa Mswima, aliyekuwa Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Mlowo kifungo cha miaka 200 jela au kulipa faini ya Mil.52, na kuamuru pia arejeshe Mil.30.8 alizoiibia halmashauri ya wilaya ya Mbozi kwa kughushi nyaraka za kutolea fedha.

Semeni Gwewa Mswima, akipanda gari la polisi baada ya kuhukumiwa kwenda jela miaka 200

Kesi hiyo ya Uhujumu Uchumi namba 01 ya mwaka 2021, ilitolewa jana Mei 7, 2021, na TAKUKURU mkoa wa Songwe mbele ya Hakimu Mkazi wa wilaya hiyo Vitalis Changwe, ambapo mshtakiwa alikuwa akikabiliwa na makosa 60 ambayo ndani yake kuna makosa ya kutumia nyaraka za uongo pamoja na wizi kwa mtumishi wa umma.

Tazama video hapa chini