
Kiongozi wa jumuiya ya Uamsho akiwa katika moja ya mikutano ya hadhara ya jumuiya hiyo kisiwani Zanzibar.
Wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, viongozi wa jumuiya hiyo Bw. Maalim Yusuph Hamis na bw. Said Amour Salim pia wamekanusha taarifa zinazoenezwa kwamba jumuiya hiyo ina mahusiano na chama cha wananchi CUF.
Wamemtaka mwenyekiti wa bunge maalum la katiba kuwachukulia hatua viongozi ambao wanahusisha suala la mchakato wa katiba na dini kwa kuwa kufanya hivyo ni kuwachanganya wananchi.