Baadhi ya Makamanda wa Polisi Zanzibar
Akizungumza na Waandishi wa Habari jana Visiwani humo Bw. Msangi amesema zoezi la kuhojiwa kwa Maalim Seif si pekee bali wataendela kufanya hivyo kwa yoyote mweye kutoa kauli ambazo zinaviashairia vya uvunjifu wa amani.
Ingawa hakueleza kwa kina undani wa mahojiano hayo na kiongozi huyo, Msangi amesema wameshamaliza kumhoji na ameachiwa kwa dhamana ya watu wawili wakati wakiwa wanaendela na uchunguzi wao juu ya matukio yanayojiri visiwani humo.
Kwa upande wake Msemaje wa Chama cha CUF, Salim Bimani ameonyeshwa kusikitishwa kwake na jeshi la Polisi Zanzibar kumhoji kiongozi huyo huku akilituhumu jeshi hilo kwa makatazo wanayoyafanya juu ya chama hicho.