Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

TAKUKURU yaokoa mamilioni ya NHIF

Jumatano , 3rd Feb , 2021

TAKUKURU mkoa wa Kagera imekabidhi zaidi ya shilingi milioni 10.3 kwa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), zilizolipwa kwa udanganyifu kwenye maduka mawili ya dawa za binadamu ambayo ni MK Pharmacy na EJU Pharmacy, baada ya kuwasilisha nyaraka za madeni wakidai kutoa huduma kwa wagonjwa.

Fedha zilizokabidhiwa na TAKUKURU kwa Mkuu wa mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti.

Akikabidhi fedha hizo mbele ya mkuu wa mkoa wa Kagera, mkuu wa TAKUKURU wa mkoa huo John Joseph, amesema kuwa fedha zilizokabidhiwa ni sehemu ya shilingi milioni 304, ambazo taasisi hiyo imeziokoa kama madeni hewa, kutokana na nyaraka zilizotumika kubainika kuwa zimeghushiwa.

Joseph amesema kuwa ufuatiliaji umebaini kuwa madai hayo yalikuwa ni ya uongo, kwa kuwa fomu za NHIF zilizowasilishwa ziliandikwa na mtu aliyeitwa Dk. Frida Samwel, ambaye sio daktari na wala hakuwahi kuajiriwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa na hatambuliki.

Akizungumzia tukio hilo mkuu wa mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti, amesema kuwa serikali haitavumilia vitendo vyovyote vya ubadhirifu, na kwamba uchunguzi dhidi ya tukio hilo unaendelea na watakaobainika watachukuliwa hatua za kisheria.

 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto