
Mbunge wa Viti Maalum, Tunza Malapo
Kauli hiyo ameitoa bungeni jijini Dodoma, hii leo Aprili 19, 2022, na kuiomba Wizara ya TAMISEMI kufuatilia pesa zinazopelekwa kwenye halmashauri kwa kuwa kuna upigaji mkubwa sana badala ya kuleta tija kwa wananchi.
"Nyinyi kama Wizara mnakazi kubwa sana ya kufuatili hizo pesa, tunaambiwa mawaziri ni vijana maana yake tunatambua mchakamchaka, vijana mnapaswa mkimbie, kama mlikuwa mnakimbia kwa spidi 100 mnapaswa mkimbie kwa spidi 150 hali huko chini sio shwari sana,"amesema Mbunge Tunza