Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

Shughuli zitakazofanyika wiki ya UKIMWI zaelezwa

Jumatano , 24th Nov , 2021

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dk. Leonard Maboko amesema katika wiki ya maadhamisho ya UKIMWI ambapo kitaifa mwaka huu inafanyika jijini Mbeya, zitafanyika shughuli mbalimbali ikiwemo Waziri Mkuu kuhudhuria Kongamano la Kisayansi juu ya mapambano ya VVU.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Tanzania (TACAIDS) Dk. Leonard Maboko

Dk. Leonard Maboko amesema hayo leo Novemba 24, 2021 kwenye uzinduzi wa wiki hiyo ambapo mgeni rasmi alikuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dk. Tulia Ackson.

''Novemba 26 tutakuwa na kongamano la kisayansi katika mapambano dhidi ya UKIMWI na kuweka mikakati. Hilo kongamano litazinduliwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa na litamalizika Novemba 27,'' ameeleza Mkurugenzi Mkuu wa TACAIDS Dk. Maboko.

Aidha, Dk. Maboko ameongeza kuwa, ''Kuna matukio mengi makubwa yatakuwa yanaendelea, wadau wote wanaoshughulika na mapambano dhidi ya UKIMWI wapo hapa kwenye mabanda. Pia kutakuwa na huduma mbalimbali ikiwemo kupima virusi vya UKIMWI, chanjo ya Uviko-19, shingo ya kizazi kwa kina mama, tohara kwa wanaume na mengine''.

Pia amesema kuwa, ''Asilimia karibu 40 ya maambukizi mapya yanatokea kwa vijana, hivyo Novemba 28, kutakuwa na Youth Dialogue, kwa vijana waliopo vyuo vikuu kujadiliana yale yanayoendelea kuhusu mapambano dhidi ya UKIMWI na ndio maana hapa kuna mabanda yanaitwa kijiji cha vijana''.

Naye Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI, Jenard Lazaro ameeleza kuwa mfuko huo umekuwa msaada mkubwa katika kutokomeza maambukizi ya virusi vya UKIMWI.

''Tangu kuanzishwa kwa Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti UKIMWI mwaka 2015, kumekuwa na mafanikio mengi ikiwemo mfuko umeweza kutoa shilingi bilioni 1.1 kununua na kusambaza dawa za  magonjwa nyemelezi kwa watu wanaoishi na VVU, '' ameeleza  Lazaro.
 

HABARI ZAIDI

Katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazini, Amani Golugwa

Maandamano yetu sio kelele za wahuni - Golugwa

Nyumba ambayo mwili wa mwanaume ulikaa hadi kuharibika

Mke aishi na maiti ya mumewe akiamini atafufuka

Ofisa wa idara ya manunuzi na mikataba akimpatia maelezo mmoja wa wananchi wawaliojitokeza kutembelea banda la GGML katika maonesho ya OSHA na kujifunza namna kuzingatia usalama katika shughuli zao za kila siku.

GGML yaja na teknolojia za kisasa za uokoaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan

Rais Samia asema CDF mwanamke atapatikana 2030

Mratibu wa idara ya dharura (ERT) kutoka GGML, Mohamed Mwaimu akimuonesha mama lishe namna ya kuzima moto wakati inatopokea mtungi wa gesi unapopata hitilafu na kulipuka. Mafunzo hayo yametolewana GGML kwa kushirikiana na OSHA kwa akina mama lishe 50 wa mkoani Arusha.

Mama lishe wafundishwa kulikabili janga la moto