Kazi ya uchimbaji ikiendelea mgodini
Rai hiyo imetolewa leo mkoani Geita na Mratibu wa Mradi wa Uondoaji Ajira Hatarishi na Vitendo vya Ukatili kwa Watoto wa shirika hilo, Maxmillian Kitigwa alipokuwa akiongea na wanahabari kuhusu changamoto zinazoukabili mradi huo.
Bw. Kitigwa amesema, katika Mkoa huo kuna changamoto nyingi zinazowakabili watoto lakini kukosekana kwa Idara ya Kazi katika maeneo ya migodi kunasababisha uvunjwaji mkubwa wa haki za watoto kwa kuwa watoto wengi wanakimbilia kufanya shughuli mbalimbali katika maeneo hayo ili kujipatia kipato.
Amesisitiza kwamba, sasa hivi Geita ni mkoa ambao u umezungukwa na migodi mikubwa hivyo Serikali haina budi kuweka Idara ya Kazi katika maeneo hayo ili kuzuia ajira za watoto pamoja na kukomesha unyanyaswaji unaofanywa kwa baadhi ya watu wanaofanya kazi huko


