Alhamisi , 1st Mei , 2014

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete amesema serikali itaongeza mshahara kwa wafanyakazi katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/2015.

Rais wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete.

Akihutubia wafanyakazi katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani kitaifa yaliyofanyika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam,rais amesema serikali itaendelea kuongeza mishahara kwa wafanyakazi wake kulingana na makusanyo ya mapato ya taifa.

Pia Rais Kikwete amesema serikali inafanya juhudi za kupunguza makato ya kodi kwa watumishi wa umma kutoka asilimia 13 ya sasa mpaka kufikia asilimia tisa.