Error message

  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 664 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 670 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 667 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 675 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Notice: Trying to access array offset on value of type null in amp_node_view() (line 679 of /home/eatv/public_html/sites/all/modules/amp/amp.module).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).
  • Warning: "continue" targeting switch is equivalent to "break". Did you mean to use "continue 2"? in include_once() (line 3493 of /home/eatv/public_html/includes/bootstrap.inc).

RC Kilimanjaro alia na TANESCO 'Toeni taarifa'

Jumatatu , 25th Jan , 2021

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira, amelitaka Shirika la umeme nchini (TANESCO), kuhakikisha wanatoa taarifa mapema kabla hawajakata umeme ili isiweze kuleta madhara kwa wananchi na wafanyabishara wakubwa.

Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Januari 25, 2021, wakati akizungumza kwenye kipindi cha SupaBreakfast cha East Africa Radio, ambapo amesimulia ni kwa jinsi gani mteja aliyekuwa analipa milioni 100 kila mwezi kama bili ya umeme, alivyoharibikiwa na mtambo wake wa kutengeneza nondo baada ya umeme kukatika.

"Nina mfanyabiashara ambaye anazalisha chuma alikuwa keshafika mbali sana, siku moja amechoma chuma chake cha kutengeneza nondo na amenunua kinu cha fedha nyingi, chuma kile kimeshayeyuka anataka sasa aanze kutengeneza nondo umeme ukakatika,  kile chuma kikawa jiwe, kinu kikafa, kipindi hicho alikuwa analipa bili ya umeme ya milioni 100 kila mwezi", amesema RC Mghwira

Aidha RC Mghwira ameongeza kuwa, "Hata kama tunazalisha umeme kidogo, TANESCO watupe taarifa, mfano mimi Meneja akinitumia message ya hitilafu na ikifika tu nawasambazia wananchi wangu, wakuu wa wilaya na wenyewe nawaambia sambazeni, nina orodha ya wazalishaji wetu wakubwa wote nawaambia jamani kutakuwa na hitilafu ya umeme"
 

HABARI ZAIDI

Dkt. Selemani Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

Hati miliki ardhi za kimila 4,450 kutolewa Mei 29

DCP David Misime, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania

Mtoto atekwa na mzazi wake ili ajipatie milioni 20

Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Anton Sabasaba Akizungumza wakati alipohudhuria kikao cha wazazi katika Shule ya Msingi Elisabane Mei 24, 2024

Wototo wafuatiliwe na kulindwa kama mboni - Anton